Latest News

Snura aomba radhi kwa wimbo uliofungiwa Tanzania

Msanii Snura Mushi ambaye wimbo wake wa Chura ulipigwa marufuku na serikali ya Tanzania ameomba radhi na kuahidi kutekeleza maagizo ya serikali.
Wimbo huo ulipigwa marufuku na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ambayo ilisema "maudhui ya utengenezwaji wa video ya wimbo huo “haiendani na maadili ya Mtanzania.”
Mamlaka hiyo ilisema kazi hiyo inadhalilisha tasnia ya muziki.
Serikali ilipiga marufuku maonyesho yote ya hadhara ya Snura hadi pale atakapokamilisha usajili wa kazi zake za Sanaa katika Baraza la Sanaa la Taifa (Basata).
Snura
Image captionSnura amewaonesha kile alichosema ni cheti
Akizungumza na wanahabari akiwa ameandamana na meneja wake, Snura amesema amechukua hatua na kusajiliwa rasmi kwa ajili ya shughuli za kisanii.

No comments:

Post a Comment

PERUZI24HOURS Designed by Templateism.com Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.