Alexis Tsipras, ametetea mageuzi ya ulipaji kodi Ugiriki, uchaguzi wa urais unafanyika Ufilipino na ‘Malkia wa Pembe za Ndovu’ atafika kortini leo Dar es Salaam.
Waziri mkuu wa Ugiriki, Alexis Tsipras, ametetea mageuzi mapya ya
mfumo wa ulipaji kodi na malipo ya uzeeni yaliyoidhinishwa na bunge.
Hatua
hizo ni mojawapo wa masharti yanayohitajika kupata fungu zaidi la
ufadhili wa kimataifa kuokoa uchumi wa taifa hilo lakini Bw Tsipras
amesema mabadiliko hayo hayatawaathiri watu wengi waliostaafu.
Mawaziri wa fedha kutoka mataifa yanayotumia sarafu ya Euro wanakutana leo Jumatatu kujadili fungu hilo la malipo.
2. Uchaguzi wa urais wafanyika Ufilipino
Image copyrightReutersImage caption
Duterte ametishia kuwaua maelfu ya wahalifu
Mamilioni ya raia wa Ufilipino wanapiga kura katika
uchaguzi wa urais ambao huenda ukashuhudia meya mwenye msimamo mkali
akichaguliwa kuwa rais mpya wa taifa hilo. Meya huyo mwenye umri wa
miaka 72, Rodrigo Duterte, amewachangamsha wapiga kura na kampeni zake
zilizojaa ugomvi ikiwemo kutishia kuwauwa maelfu ya wahalifu.
3. Washukiwa wanne kushtakiwa Honduras
Image copyrightGettyJaji mmoja nchini Honduras ameamua kuwa wanaume
wanne wanaweza kufunguliwa mashtaka ya mauaji ya mwanaharakati wa
mazingira, Berta Caceres.
Baadhi ya watu hao ni wanajeshi
waliostaafu na wengi bado wanahudumu jeshini. Wengine wameajiriwa na
kampuni zinazojenga bwawa kubwa la kuzalisha umeme ambalo ujenzi wake Bi
Caceres na vuguvugu la wenyeji limekuwa likipinga.
4. Seoul yapuuza pendekezo la Korea Kaskazini
Image copyrightAFPImage caption
Kim amependekeza nchi hizo mbili zikutane kwa mazungumzo
Serikali ya Korea Kusini imepuuza na kulitaja kuwa
propaganda ya kinafiki pendekezo la Korea Kaskazini kwamba mataifa hayo
mawili yanapaswa kukutana kufanya mazungumzo.
Tamko hilo linafuatia tangazo la kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong-un, katika kongamano la chama tawala cha Workers Party.
Lakini baadaye kongamano hilo liliidhinisha azimio linaloimarisha uwezo wa Pyongyang kujihami kwa silaha za nyuklia.
5. Wanauchumi wapinga mataifa nafuu kwa kodi
Image copyrightAFPImage caption
Mkutano wa kupambana na ufisadi utafanyika baadaye wiki hii London
Zaidi ya wanauchumi 300 wametia saini barua kwa
waziri mkuu wa Uingereza David Cameron pamoja na viongozi wengine
duniani wakisema hakuna sababu zaidi za kuendelea kuwepo maeneo ya
kuhifadhi pesa za kigeni kwa ajili ya kukwepa kulipa kodi. Ujumbe wao
unakuja kabla ya mkutano wa kupambana na ufisadi mjini London baadaye
wiki hii.
6. Malkia wa Pembe za Ndovu kufika kortini Tanzania
Image copyrightAFPNa mfanyibiashara mmoja wa kichina mwanamke
anatarajiwa kufikishwa mahakamani nchini Tanzania hivi leo kufunguliwa
mashtaka ya kuendesha mtandao wa kihalifu uliokuwa ukisafirisha
kimagendo pembe za ndovu hadi barani Asia.
Viongozi wa mashtaka
wamesema kuwa Yang Feng Glan, ambaye anajulikana kwa jina la utani kama
Malkia wa pembe za ndovu aliongoza biasha haramu iliyowauwa ndovu katika
mbuga za wanyama.
Amekanusha mashtaka hayo.
No comments:
Post a Comment