Latest News

Migiro ateuliwa balozi wa Tanzania Uingereza



Mmoja wa wanasiasa waliokuwa wakipigania tiketi ya kuwania urais kupitia chama cha CCM nchini Tanzania ameteuliwa kuwa balozi wan chi hiyo Uingereza.
Dkt Asha-Rose Migiro atachukua nafasi iliyoachwa wazi na Bw Peter Kallaghe ambaye amerejea nyumbani.
Anatarajiwa kuapishwa Alhamisi katika ikulu ndogo ya rais Dodoma.
Bi Migiro alihudumu kama Waziri wa Katiba na Sheria serikali iliyopita na alikuwa miongoni mwa wagombea watatu waliokuwa wamesalia kwenye kinyang'anyiro cha kuteua mgombea wa CCM uchaguzi wa mwaka jana, kabla ya mwishowe Dkt John Magufuli kuidhinishwa.
Mgombea huyo mwingine alikuwa Balozi Amina Salum Ali.

No comments:

Post a Comment

PERUZI24HOURS Designed by Templateism.com Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.