Latest News

Mafuriko zaidi yatishia Paris Ufaransa


Utawala nchini Ufaransa uko katika hali ya tahadhari kuu baada ya mvua kubwa kunyesha katika maeneo ya milima na kutishia kusababisha mafuriko zaidi.
 
Mto Seine unatarajiwa kuvunja kingo zake na kusababisha mafuriko katika muda mchache ujao.

Mabarabara kadha na reli na hata daraja chache zimefungwa katika maandalizi ya kupambana na mafuriko hayo yanayotarajiwa.

Wenyeji wa maeneo mengi yaliyochini na karibu na mto huo tayari wamelazimika kuhama makwao.

Tahadhari hiyo kuu inatokana na vifo vya takriban watu 10 katika siku tatu zilizopita nchini humo na Ujerumani ambayo pia imeathirika vibaya na mafuriko hayo.

Miji kadhaa Kusini mwa Ujerumani imeharibiwa sana na mafuriko.

Wafanyakazi wa umma wameweka vizuizi kadhaa katika kingo za mito na wakaazi wengine katika mji mmoja wamelazimika kutumia boti kusafiri kutoka manyumbani mwao.

Rais wa Ufaransa, Francois Hollande, ametaja hali ya hewa kama mabadiliko yanayohusiana na mabadiliko makubwa kote duniani.

No comments:

Post a Comment

PERUZI24HOURS Designed by Templateism.com Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.