DAR
ES SALAAM
Ofisi ya Taifa Ya Takwimu NBS imesema kuwa mfumuko wa bei wa
Taifa Kwa mwezi Januari 2018 umebaki kuwa asilimia 4.0 kama ilivyokuwa mwezi
disemba 2017.
Akizungumza na vyombo vya habari jijini Dar es salaam Mkurugenzi
wa Sensa ya Watu na Takwimu za Jamii EPHRAIM
KWESIGABO amesema takwimu hizo zinaonesha kuwa kasi ya mabadiliko ya bei za
bidhaa na huduma kwa mwaka ulioisha mwezi Januari 2018 umekuwa Sawa na kasi ya
mwaka 2017.
KWESIGABO amefafanua kuwa mfumuko wa bei wa Taifa
unapima kiwango cha kasi cha mabadiliko ya bei za bidhaa na huduma zote
zinazotumiwa na Kaya binafsi hapa nchini.
amesema bei za baadhi za vyakula zilizochangia mfumuko wa bei
kufikia asilimia 4.0 Kati ya mwezi januari 2017 hadi januari 2018 ni pamoja na
mahindi ,maharage , samaki na ndizi za kupika.
Ofisi ya Taifa ya Takwimu NBS ni taasisi ya umma
iliyoanzishwa Kwa sheria ya Takwimu mwaka 2015 iliyopewa mamlaka ya kutoa,
kusimamia na kuratibu upatikanaji wa Takwimu rasmi nchini.
Na. ASHURA DUNDA
No comments:
Post a Comment